Showing posts with label Swahili. Show all posts
Showing posts with label Swahili. Show all posts

Monday, January 21, 2019

Ati Twonane Mtoni

1.Ati twonane mtoni?
Maji mazuri ya Mbingu;
Yanatokea mwangani,
Penye kiti cha Mungu.

Naam, twonane mtoni!
Watakatifu, kwenu ni mtoni!
Tutakutanika mtoni
Penye kiti cha Mungu
.
2.Tukitembea mtoni
Na Yesu mchunga wetu
Daima tu ibadani
Usoni pake kwetu.
3.Kwang’ara sana mtoni
Cha Mwokozi ni kioo,
Milele hatuachani,
Tumsifu kwa nyimbo.
4.Si mbali sana mtoni,
Karibu tutawasili,
Mara huwa furahani
Na amani ya kweli.

Sunday, January 20, 2019

Anipenda ni Kweli

1.Anipenda ni kweli;
Mungu anena hili;
Sisi wake watoto;
kutulinda si zito.
Yesu anipenda,
Yesu anipenda,
Kweli anipenda,
Mungu amesema.
2.Kwa kupenda akafa
Niokoke na kufa;
Atazidi taka,
Sana ataniweka.
3.Anipenda kabisa;
Niuguapo sasa
Anitunza Mbinguni
Nniliyelala chini.
4.Kunipenda haachi,
Tu sote hapa chini
Baada ya mashaka
Kwake tanipeleka.

Thursday, October 11, 2018

Dhambi Ikikulemea


Dhambi ikikulemea,
Kwa Bwana rehema;
Hivi sasa tegemea
Neno la salama.

Tegemea, tegemea,
akwita sasa.
Ni Mwokozi,
Ni Mwokozi; amini sasa.

Yesu amemwaga damu
Ya nyingi baraka;
Nawe sasa oga mumu
Zioshwamo taka.

Ni njia yeye hakika
Hwongoza rahani;
Usikawe kumshika,
Uwe barakani.

Karibu nawe wingie
Mwetu safarini,
Twende tukamwamkie,
Milele Mbinguni.

Thursday, November 7, 2013