1.Akifa Yesu nikafa naye
Uzima upya huishi naye;
Humtazama mpaka nje:
Nyakati zote ni wake yeye.
Uzima upya huishi naye;
Humtazama mpaka nje:
Nyakati zote ni wake yeye.
Nyakati zote nimo pendoni,
Nyakati zote ni uzimani,
Humtazama hata atokee,
Nyakati zote mimi ni wake.
Nyakati zote ni uzimani,
Humtazama hata atokee,
Nyakati zote mimi ni wake.
2. Vita sipigi visivyo haki,
Na Bwana wangu hapiganiki;
Beramu yake haitwaliki,
Napo po pote hila sitaki.
Na Bwana wangu hapiganiki;
Beramu yake haitwaliki,
Napo po pote hila sitaki.
3. Sina mashaka, akawa mbali;
Mizigo yote aihimili;
Ananituliza Imanweli,
Nyakati zote mimi husali.
Mizigo yote aihimili;
Ananituliza Imanweli,
Nyakati zote mimi husali.
4. Sina huzuni na mimi sidhii;
Simwagi chozi, wala siguni;
Sikuti afa, ila kitini
Daima hunifikiri mimi.
Simwagi chozi, wala siguni;
Sikuti afa, ila kitini
Daima hunifikiri mimi.
5. Kila unyonge huusikia;
Kila ugonjwa kwake hupoa;
Yesu ni mwenye kuniokoa
Nyakati zote hunijalia.
Kila ugonjwa kwake hupoa;
Yesu ni mwenye kuniokoa
Nyakati zote hunijalia.
0 comments:
Post a Comment