Nionapo amani kama shwari, ama
nionapo shida;
Kwa mambo yote umenijulisha, ni
salama rohoni mwangu.
Salama, rohoni
Ni salama rohoni mwangu
Ingawa shetani atanitesa,
nitajipa moyo
kwani Kristo ameona unyonge
wangu, amekufa kwa roho yangu.
Dhambi zangu zote, wala si nusu,
zimewekwa msalabani;
Wala sichukui laana yake, ni
salama rohoni mwangu.
Ee Bwana himiza siku ya kuja,
panda itakapolia;
utakaposhuka sitaogopa, ni salama
rohoni mwangu.
0 comments:
Post a Comment