1.Anisikiaye, aliye yote;
Sasa litangae, wajue wote,
Duniani kote neno wapate,
Atakaye na aje!
Sasa litangae, wajue wote,
Duniani kote neno wapate,
Atakaye na aje!
Ni “Atakaye”, ni “atakaye”,
Pwani hata bara, na litangae;
Ni Baba Mpenzi alinganaye
Atakaye na aje.
Pwani hata bara, na litangae;
Ni Baba Mpenzi alinganaye
Atakaye na aje.
2.Anijiliaye, Yesu asema,
Asikawe, aje hima mapema;
Ndimi njia, kweli, ndimi uzima;
Atakaye na aje!
Asikawe, aje hima mapema;
Ndimi njia, kweli, ndimi uzima;
Atakaye na aje!
3.Atakaye aje, ndivyo ahadi;
Atakaye hiyo, haitarudi!
Atakaye lake, ni la abadi!
Atakaye na aje.
Atakaye hiyo, haitarudi!
Atakaye lake, ni la abadi!
Atakaye na aje.
0 comments:
Post a Comment